Monday, January 16, 2012

HABARI


                          Rais wa  chama cha madaktari  Tanzania ,bw .Mkopi.                                      

Chama cha Madaktari nchini (MAT), kimetoa muda wa saa 72 kwa serikali kuwarejesha kazini madaktari waliofukuzwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam wanarejeshwa kazini mara moja.
Taarifa ya chama hicho imesisitiza kwamba, ikiwa  serikali haitotekeleza matakwa yao, basi kitaitisha mkutano mwingine siku ya Jumatano wiki hii, kujadili mambo mbalimbali likiwemo suala la kufukuzwa kwa  madaktari hao.
Chama hicho  pia kimemtaka Rais Jakaya Kikwete, kumwajibisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Blandina Nyoni kwa kuwa chanzo cha migogoro ya madaktari hapa nchini.
Mgogoro huo wa madakatari na serikali unafuatia kufukuzwa kwa wenzao 229 baada ya kuitisha mgomo wa kudai posho zao ambapo walilipwa na serikali lakini baadaye wakapewa barua za kufukuzwa kazi.

No comments: