Friday, January 27, 2012

MGOMO WASAMBAA!

 Waziri wa afya Dk.Hajji Mponda na naibu wake Dk Lucy Nkya


DAR ES SALAAM         

Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk Haji Mponda amewataka madaktari walioko kwenye mgomo kurejea kazini ili kuoko maisha ya watanzania wakati  hoja zao zikifanyiwa kazi na serikali.

Waziri Mponda ameyasema hayo jijini Dar es salaam na kuwasihi madktari kufanya mpango wa kufika ofisi ya waziri mkuu kwa ajili ya majadiliano,huku pia akisisitiza kwamba kanuni za utumishi zinamtaka mtumishi kudai haki yake huku akiwa anaendelea na majukumu yake kama kawaida.

Mgomo huo wa madaktari ambao unaingia siku ya nne hii leo,tayari umesambaa katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo mikoa ya mwanza,na mbeya.

Kwa upande wao madaktari wameitaka serikali kutumia njia sahihi kujibu hoja zao za msingi ili kuleta suluhu ya suala hilo.

Mwenyekitiwa madaktari hao  Dk Steven Ulimboka ameitaka serikali kuchukua hatua za haraka katika kuhakikisha kwamba madai yao yanafanyiwa kazi kabla ya kutokea kwa athari kubwa zaidi.

Katika hatua nyingine,wakati serikali ikiwataka madaktari kurejea kazini ili kuokoa maisha ya watanzania wanaotegemea huduma zao, Mkoani Kilimanjaro madaktari zaidi ya 100 katika hospitali ya rufaa ya KCMC wamekubaliana  kuanza mgomo wao hii leo asubuhi kuunga mkono wenzao ambao wako katika mgomo.

Madaktari hao wamefikia maamuzi hayo hapo jana jioni katika kikao walichofanya katika ukumbi wa hospitali hiyo kujadilia madai yanayodaiwa na wenzao walioanza mgomo jijini dare s salaam.

Wakizungumza mara baada ya kikao hicho ,  wamesema madai ya wenzao ambao wako katika mgomo ni ya msingi ,na kwamba hayapaswi kupuuzwa kwa namna yoyote .

Wamesisistiza kwamba wataingia katika mgomo na kuwaunga mkono wenzao hadi pale serikali itakapochukua hatua  mahususi ikiwa ni pamoja na kuwasikiliza na kuyatafutia ufumbuzi madai yao.
......................................................................................................................................................................






DAR ES SALAM              

SERIKALI imesema imefanikiwa kukusanya mapato yanayotokana na kodi mbalimbali kwa zaidi ya asilimia 100 kutokana na ushirikiano mzuri baina ya wananchi serikali na ,idara mbalimbali.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati akijibu maswaliya  waandishi wa habari mara baada ya kufungua mkutano wa siku mbili wa Mazungumzo wa mwaka kuhusu Sera ya Taifa unaoendelea   jijini Dar es Salaam.
Waziri mkuu PINDA amesema katika kipindi cha miezi  3 seriklai imefanikiwa kukusanya mapato ya kodi kwa zaidi ya asilimia 100 kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali vya mapato nchini.
Akizungumzia kuhusu mkutano huo, Waziri Mkuu, amesema lengo kubwa ni kufanya tathimini na kuangalia mipango mbalimbali ya maendeleo ikiwa imetekelezwa au la.




 Waziri mkuu akiwa na mabalozi na mawaziri katika mkutano huo.

.........................................................................................................................................................................
ARUSHA                     

Jeshi la polisi mkoani Arusha limeombwa kukidhibiti kikundi kinachojiita jeshi la kimila kilichoundwa wilayani Arumeru ili kuepusha kutokea kwa ghasia baina ya wananchi na kikundi hicho.

Wakizungumza na kituo hiki wananchi wilayani arumeru  wamesema kikundi hicho hufanya shughuli zake nyakati za usiku ikiwemo kuwakamata wananchi kuwapiga na kuwafanyia vitendo vya udhalilishaji.

Kiongozi wa wananchi hao SAIBOKO NGOISO ameliomba jeshi la polisi kudhibiti kikundi hicho haraka kabala ya wananchi kuamua kujichukulia sheria mikononi hali mabnbayo inaweza kusababisha umwagaji damu.

Malalamiko  ya wananchi hao yanajuka siku chache mara baada ya viongozi mbalimali wa serikali  akiwemo naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi GOODLUCK OLE MEDEYE  kusema kwamba kwa serikali inaendelea kushughulikia suala hilo ,huku pia akiwataka wananchi walioyakimbia makazi yao kurejea nyumbani.

No comments: