Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akipunga
mkono kusalimia wananchi wakati akiingia Uwanja wa Uhuru jijini Dar es
Salaam leo Aprili 26, 2012 katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 48 ya
Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
Vikosi vya Ulinzi na Usalama vikipita na kutoa heshima mbele ya jukwaa
kuu kwa mwendo wa pole na haraka, wakati wa maadhimisho ya sherehe hizo
leo.
Haraiki ya wanafunzi wapatao 1,727 kutoka shule za msingi mbalimbali Tanzania bara na visiwani wameipamba vizuri sherehe ya maadhimisho ya
miaka 48 ya Muungano wa Tanzania
yaliyofanyika leo katika viwanja vya Uhuru
jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Viongozi wa Kiserikali wakiwa ni miongoni mwa
waliohudhuria sherehe hizo katika Uwanja wa Uhuru, wakisimama wakati wa
kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Baadhi ya Viongozi wa Kiserikali wakiwa ni miongoni mwa
waliohudhuria sherehe hizo katika Uwanja wa Uhuru, wakisimama wakati wa
kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
akikagua vikosi vya ulinzi na usalama wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya miaka
48 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es
Salaam leo




No comments:
Post a Comment