Thobias Andengenye, Kamanda wa polisi mkoa waArusha
Kamanda wa
polisi mkoa wa Arusha Thobias Andengenye ametolea ufafanuzi suala la kuisaidia
polisi na kusema kuwa si kila anayeisaidia polisi analazimika kukaa selo.
Akizungumza
katika mahojiano maalum na Radio 5 kamanda Andengenye amesema suala lililopo ni
aina ya ushahidi unaotafutwa na polisi na kuongeza kuwa watu wengi wanaisaidia
polisi na wako nyumbani.
Mkuu huyo wa
polisi ameeleza kuwa endapo mtu atatakiwa kuisaidia polisi na ushahidi wake
umsaidie kumsafisha au kumtia hatiani mtu huyo huwekwa ndani kulinda taarifa
ambazo polisi inakuwa nazo.
Kituo hiki
kiliamua kutafuta ufafanuzi wa suala hilo kutokana na maswali ambayo watu
wamekuwa wanahoji kuhusu mtu kuisaidia polisi kwanini anawekwa chini ya ulinzi
wa jeshi hilo.

No comments:
Post a Comment