Waziri mkuu mh.Mizengo Pinda.
DAR ES SALAAM:
Madaktari katika baadhi ya maeneo nchini
wameendelea na mgomo wao licha ya agizo la waziri mkuu kuwataka kurejea katika
vituo vyao vya kazi hapo jana ,na kwamba atakayeshindwa kufanya hivyo atakuwa
amejiondoa mwenyewe katika utumishi wa
uma.
Katika hopsitali ya taifa muhimbili jijini
dar es salaam mgomo wa madaktari
umeendelea kama kawaida hapo jana ,huku hali ya wagonjwa waliokuwa hospitalini
hapo ikizidi kuwa mbaya na baadhi yao kufariki dunia.
Hata hivyo mgomo huo umeendelea kuchukua sura
mpya baada ya wauguzi katika hospitali hiyo kungana na madakatari katika mogomo
huku baadhi yao wakipinga hatua ya kutaka kuletewa madaktari kutoka jeshini.
Katika baadhi ya mikoa ikiwemo Mbeya , Mwanza
na Kilimanjaro baadhi ya madaktari wameonekaana kusaini vitabu vya mahudhurio
na kuondoka bila ya kuwahudumia wagonjwa.
No comments:
Post a Comment