Tuesday, January 10, 2012


           
                                                 Mkurugenzi wa Nssf DR.Ramadhan Dau.

JAN 10, 2012                                      

Serikali imesaini mkataba na shirika la hifadhi ya jami NSSF kwaajili ya ujenzi wa daraja la Kigamboni jijini dar es salaam.

Mkurugenzi mkuu wa NSSF dakta Ramadhan Dau amesema ujenzi wa daraja hilo ambao unatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni mia 2,utakamilika katika kipindi cha miaka mitatu.

Ameongeza kwamba ujenzi huo utatekelezwa kwa ushirikiano baina ya wakandarasi wa hapa nchini na china.

Kwa upande wake waziri wa ujenzi Dakta  JOHN MAGUFULI amewataka wakandarasi hao kutekeleza ujenzi huo kwa wakati na pia katika kiwango kinachotakiwa.


.......................................................................................................................................


 Katibu mkuu wa baraza la mitihani Dr. joyce ndalichako



  JAN 10,2012                                                    

Wanafunzi elfu tisa waliofutiwa matokeo ya kuhitimu elimu ya msingi mwishoni mwa mwaka jana wanataraji kurudia mtihani huo mwaka huu mwezi September.
Naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi PHILIP MULUGO ametoa kauli hiyo katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Naibu waziri MULUGO amesema hatua hiyo ya serikali inalenga kuwapa  fursa nyingine wanafunzi ambao wamepoteza nafasi ya kujiunga na elimu ya sekondari  mara baada ya kufutiwa matokeo  yao.
Katika hatua nyingine MULUGO amesema utaratibu wa kawaida utatumika kuwahamisha wanafunzi walioathirika na janga la mafuriko jijini dare s salaam,na kuwapatia nafasi  katika shule za jirani na makazi yao mapya watakayo hamia.




 .....................................................................................................................................

 Maalim Seif  kushotom akiwa na mwenyekiti wa chama cha wana nchi (CUF) Prf.Ibrahim lipumba.


ZANZIBAR:         JAN 10, 2012                      SAA   1 ASUBUHI

Makamu wa kwanza wa rais wa zanzibar MAALIM SEIF HAMAD amesema wakati umefika kwa wazanzibar kuacha  utegemezi kwa wahisani katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo.
Maalim Seif ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa jengo la Mfuko wa Barabara lililogharimu zaidi ya shilingi millioni mia 6   Mjini Unguja ambalo limebuniwa na kujengwa na wataalam wazalendo.
Amesema iwapo kutakuwa na jitihada za makusudi katika kupanga mipango kwa mujibu wa hali ya kifedha wataweza kutekeleza miradi ya kimaendeleo kwa uhakika na haraka.
Maalim seif Amesema ujenzi wa jengo hilo umegharamiwa na Mfuko wenyewe bila ya kutegemea wafadhili na kujengwa kwa muda wa chini ya mwaka mmoja.









No comments: