Waziri Nchimbi .
Waziri
wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali
inakubali kuwa wastaafu kupewa mkataba wa kuendelea kufanya kazi si sahihi na
kuahidi kuwa suala hilo litafanyiwa kazi.
Akifanya
majumuisho wakati wa mjadala wa Azimio la kuridhia mkataba wa vijana wa Afrika
(The African Youth Charter) waziri Nchimbi alisema hatua ya wastaafu kupewa
mikataba ya kuendelea na kazi inawanyima vijana haki ya kupata ajira katika
taasisi mbalimbali.
Akizungumzia
suala la maadili kwa vijana Mheshimiwa Nchimbi alisema hivi sasa vijana
wakiwemo baadhi ya viongozi wanaotoa michango yao juu ya mambo mbalimbali
katika mitandao kama vile facebook na twitter wanatumia lugha zisizojenga na
badala yake aliwataka kutoa michango isiyokuwa na madhara kwa vijana wa taifa
hili hasa ile inayotumia lugha zinazojenga ili kulinda maadili ya Mtanzania.
Aliwataka
viongozi kuwa wa kwanza kupiga vita matumizi mabaya ya mitandao na kuacha tabia
za kulipiza visasi pale wanapokosana na wenzao kwani hizo si sifa za kiongozi
bora. “kiongozi bora na imara ni yule mwenye tabia ya kusamehe, alisema”.
Kuhusu
mchakato wa kutafuta vazi la taifa waziri huyo alisema wizara yake inatekeleza
maagizo yaliyotolewa na bunge na kuwaomba wabunge kuwa wa kwanza kuunga mkono
wizara ya habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inapotekeleza maagizo hayo.
Aliongeza kuwa kamati iliyoteuliwa kutafuta vazi la taifa ni makini kwa kuwa
imeundwa na watu makini waliotoka kwenye kada mbalimbali.
Awali
akichangia mjadala huo, Mbunge wa Kigoma Mjini (CCM) Peter Serukamba alisema
suala la wastaafu kupewa mkataba wa kuendelea na kazi halifai kwa kuwa
linawanyima vijana haki yao ya kupata ajira. Alitoa mfano kuwa hivi sasa
wenyeviti wa bodi wengi ni wastaafu ambapo ilipaswa nafasi hizo kuchukuliwa na
vijana.
.jpg)
No comments:
Post a Comment