Friday, February 3, 2012

SIKU YA SHERIA

RAIS Jakaya Kikwete, ameagiza mahakama nchini kuhakikisha unatoa elimu kuhusu adhabu mbadala ya kifungo katika kesi za jinai.
Hatua hiyo imeelezwa kuwa itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza msongamano wa wafungwa na mahabusu magerezani.
 Rais Kikwete, ametoa wito huo jana katika sherehe za Siku ya Sheria Nchini, iliyofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Siku ya sheria ni ishara ya ufunguzi rasmi wa shughuli za mhimili huo kwa mwaka huu, chini ya kauli mbiu ya ‘Adhabu mbadala ya kifungo katika kesi za jinai faida kwa jamii’.
Rais  amesema mbali na kupunguza msongamano, pia kutawafanya wahalifu waliofungwa vifungo vya nje kuwa karibu na jamii na kufanya shughuli nyingine za jamii, hivyo kujirudi kitabia.

No comments: